Like Us On Facebook
Follow Us on Twitter

Mama Kanumba Atoa La Moyoni, Baada Ya Hukumu Ya Lulu

Mama wa Muigizaji Marehemu Steven Kanumba, Flora Mtegoa ametoa neno baada ya hukumu ya msanii wa Bongo movie Elizabeth Michael maarufu kama Lulu kutolewa, amesema kuwa leo atakwenda makaburi ya kinondonni alipoziikwa mwanaye ili kwenda kumzika upya.
Mama Kanumba ametoa kauli hiyo muda mfupi baada ya Mahakama Kuu kumhukumu kifungo cha miaka miwili Muigizaji Elizabeth Michael ambaye alikuwa mtuhumiwa katika kesi ya mauaji bila kukusudia yaliyopelekea kifo cha muigizaji huyo.
Usipitwe na Habari Muhimu, Install App  Yetu


Android ===>  Bofya hapa
“Kwa sasa sina la kusema ila  naishukuru sana Mahakama kwa kutenda haki, pia niishukuru sana Serikali yangu lakini pia nikitoka hapa nitakwenda makaburini kwa ajili ya kumzika upya mwanangu Kanumba”. Mama Kanumba.
Kwa upande wa Wakili wa Muigizaji Lulu, Peter Kibatala ameweka wazi kwamba watakata rufaa kufuatia hukumu ya Mahakama iliyotolewa leo kwa mteja wake.
Muigizaji Lulu leo amehukumiwa kifungo cha miaka miwili jela baada ya kukutwa na hatia ya kumuua muigizaji mwenzake ambaye pia alikuwa mpenzi wake Steven Kanumba usiku wa Aprili 7 2012.

Bonyeza HAPA Kudownload Applicationi Ya Mawingu Blog Kwenye Simu Yako Ili Kupata Habari Zetu Haraka

===

Tupe Maoni Yako Hapa Chini
 

Mawingu Blog | Home Of Newz Copyright © 2017