Like Us On Facebook
Follow Us on Twitter

Taarifa Maalum Kuhusu Majeruhi Wa Lucky Vicent

Mbunge wa Singida Kaskazini, Lazaro Nyalandu amesema kuwa majeruhi wa shule ya Lucky Vicent ya jijini Arusha ambao walikuwa nchini Marekani kimatibabu kufuatia ajali iliyotokea jijini Arusha wako tayari kurejea nyumbani nchini Tanzania.
Hayo yamebainishwa leo na mbunge Nyalandu kupitia mtandao wake instagram ambapo amekuwa akitoa huku akiwashukuru Watanzania wote kwa sala na dua.
Ready To come home! Watoto wetu Doreen, Sadia na Wilson sasa wako tayari kurejea nyumbani. Mungu awabariki wote kwa Sala na Dua zenu. Hakika Mungu akitaka kukubariki, hakuna awezaye kuzuia! Amani iwe nao! Sote tujimuike kuwapokea KIA asubuhi saa 3.00 Ijumaa ya wiki hii. Ndege aina ya DC-8 itawarejesha nchini, na watu wote wanatarajiwa Kufika airport saa 7 asubuhi. Mgeni Rasmi atafika saa 2 asubuhi, na watoto watatua saa 3 asubuhi. Leo ntatoa RATIBA nzima ya HAFLA ya airport KIA.

Bonyeza HAPA Kudownload Applicationi Ya Mawingu Blog Kwenye Simu Yako Ili Kupata Habari Zetu Haraka

===

Tupe Maoni Yako Hapa Chini
 

Mawingu Blog | Home Of Newz Copyright © 2017