Like Us On Facebook
Follow Us on Twitter

Rooney asepa na Wachezaji wanne wa Bongo




Mkurugenzi wa Uendeshaji wa SportPesa Tanzania, Abbas Tarimba amesema wanatarajia kuandaa mpango maalumu wa kuwasaidia wachezaji wa hapa nchini angalau wanne kila mwaka kwenda England kwa ajili ya kufanya majaribio ya kucheza soka la kulipwa.

“Tunataka soka la Tanzania ilipige hatua ili siku moja na sisi tuwe na wachezaji wanaocheza  katika Ligi Kuu England.


 “Tunajipanga ili tuweze kuleta maskauti hapa nchini kwa ajili ya kuangalia wachezaji na ikiwezekana angalau kila mwaka Watanzania wanne waweze kwenda England kwa ajili kufanya majaribio ya kucheza soka la kulipwa ili siku moja tuweze kuwaona wakipambana na akina Rooney katika ligi kuu ya nchi hiyo,” alisema Tarimba.

Bonyeza HAPA Kudownload Applicationi Ya Mawingu Blog Kwenye Simu Yako Ili Kupata Habari Zetu Haraka

===

Tupe Maoni Yako Hapa Chini
 

Mawingu Blog | Home Of Newz Copyright © 2017