Like Us On Facebook
Follow Us on Twitter

Haya Hapa Makundi Ya CECAFA Challenge CUP Na Tarehe Ya Kuanza Mashindano

Tanzania Bara itafungua mashindano ya Kombe la Chalenji Desemba 3 kwa kuivaa Libya kwenye Uwanja wa Kisumu, Kenya.


Kwa mujibu wa ratiba iliyotolewa leo Alhamis na Baraza la Vyama vya Soka vya Afrika Mashariki na Kati (Cecafa) ,Tanzania Bara imepangwa Kundi A pamoja na ndugu zake Zanzibar, Rwanda, wenyeji Kenya na Libya wakati Kundi B lina timu za Burundi, Ethiopia, Uganda, Sudan Kusini na Zimbabwe.

Libya na Zimbabwe zimealikwa kushiriki mashindano hayo baada ya Sudan na Somalia kujiondoa kwa sababu mbalimbali

Bonyeza HAPA Kudownload Applicationi Ya Mawingu Blog Kwenye Simu Yako Ili Kupata Habari Zetu Haraka

===

Tupe Maoni Yako Hapa Chini
 

Mawingu Blog | Home Of Newz Copyright © 2017