Like Us On Facebook
Follow Us on Twitter

Kamati Ya Saa 72 Kuzikalia Kikao Penalti Za Simba

Wachezaji wa Yanga na Simba mchezo ukiendelea.
KAMATI ya Saa 72 ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) inatarajia kukutana wakati wowote kuanzia sasa kwa ajili ya kujadili madai ya Simba kunyimwa penalti katika mechi kadhaa ikiwa ni pamoja na mambo mbalimbali yaliyojitokeza katika mechi za hivi karibuni.

Simba kupitia msemaji wake, Haji Man­ara wamelalamika juu ya waamuzi ku­wadhurumu kwa kutowatendea haki ka­tika mechi tatu kwa kuwanyima na kutoa penalti ambayo si halali.



Mwenyekiti wa Kamati ya Waamuzi, Salum Chama amesema madai ya Simba yatafikishwa katika Kamati ya Saa 72 ili kupitia mechi husika kama ilivyo taratibu walizojiwekea.
“Manara ametumia haki yake ya msingi kusema vyovyote anavyojisikia kwa mu­jibu wa kanuni na sheria ya nchi ilimradi asivunje sheria.
Usipitwe na Habari Muhimu, Install App  Yetu

Android ===>  Bofya hapa
“Sisi kama kamati ya waamuzi tunaona waamuzi wetu wa­nachezesha sawa kwani kwenye soka kuna kushin­da, kufungwa na kutoa sare, hoja ya kunyimwa penalti siyo kweli, na si kila mpira unaompiga mchezaji ni penalti, mwamuzi ndiye anayeamua.

“TFF ina kamati watapitia vi­pande vya video za michezo inayolalamikiwa na kuanga­lia maeneo yote yenye mata­tizo katika mechi zilizochezwa na iwapo tutabaini upungufu wowote tutachukua hatua kwa mujibu wa kanuni tuliyo­jiwekea katika kamati yetu,” alisema Chama.

Bonyeza HAPA Kudownload Applicationi Ya Mawingu Blog Kwenye Simu Yako Ili Kupata Habari Zetu Haraka

===

Tupe Maoni Yako Hapa Chini
 

Mawingu Blog | Home Of Newz Copyright © 2017