Like Us On Facebook
Follow Us on Twitter

Samatta Afanyiwa Upasuaji Kwa Saa Moja Ubelgiji


MSHAMBULIAJI wa kimataifa wa Tanzania, Mbwana Ally Samatta amefanyiwa upasuaji wa goti leo mjini Genk, Ubelgiji baada ya kuumia wiki iliyopita na sasa anaanza safari ya kuishi wiki sita na zaidi bila kufanya mazoezi.
Akizungumza na Bin Zubeiry Sports – Online leo, Samatta amesema kwamba upasuaji huo ulidumu kwa saa moja na baada ya hapo akarejea nyumbani kwake kwa kiti maalum cha kutembelea walevamu, au wagonjwa wasiojiweza kutembea.
“Napenda kuwajulisha kuwa operesheni yangu imeenda vizuri. Napenda kumshukuru Mwenyezi Mungu, timu ya madaktari pamoja na mashabiki wangu. Nimepokea meseji nyingi sana kutoka sehemu tofauti duniani na napenda kuchukua fursa hii kuwashukuru sana kwa meseji na dua zenu,”amesema Samatta.


Mbwana Samatta amefanyiwa upasuaji kwa saa moja leo mjini Genk baada ya kuumia wiki iliyopita


Samatta aliumia goti Jumamosi ya Novemba 4, mwaka huu akiichezea klabu yake, KRC ikilazimishwa sare ya 0-0 Jumamosi na Lokeren katika mchezo wa Ligi Daraja la Kwanza A Ubelgiji Uwanja wa Luminus Arena mjini Genk.
Na baada ya kufanyiwa vipimo ikagundulika Samatta ameumia kwenye mishipa midogo ya goti lake la mguu wa kulia ambayo ilichanika, hivyo kuhitaji kufanyiwa upasuaji mdogo ili apone sawia.
Samatta aliumia akiichezea mechi ya 70 Genk tangu alipojiunga nayo Januari mwaka 2016 akitokea TP Mazembe ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC).
Na katika mechi hizo 70, Samatta, mshambuliaji wa zamani wa Mbagala Market, African Lyon na Simba za Tanzania, amefunga mabao 22 kwenye mashindano yote.

Bonyeza HAPA Kudownload Applicationi Ya Mawingu Blog Kwenye Simu Yako Ili Kupata Habari Zetu Haraka

===

Tupe Maoni Yako Hapa Chini
 

Mawingu Blog | Home Of Newz Copyright © 2017