Like Us On Facebook
Follow Us on Twitter

Haya Ndio Madhara 12 ya Kujichubua Ngozi


Tabia ya kujichubua ilianza kupata umaarufu kwanzia mika ya 1980 mpaka miaka ya hivi karibuni, hii hasa kwenye nchi za watu ambao hawana ngozi nyeupe kabisa kama waarabu, wahindi na waafrika. biashara hii imewafanya watu wanaotengeneza bidhaa hizi kua matajiri sana huku zikiacha madhara makubwa kwa watumiaji.
kitaalamu  matibabu dawa kujichubua yalitakiwa yatolewe kitaalamu kwa ajili ya kuondoa mabaka ya ngozi na kuondoa makunyazi ya uzee lakini chini ya usimamizi maalumu wa daktari na matumizi yake yawe ya muda fulani tu kama dozi ya dawa lakini hali hii imekua tofauti kwani kemikali hizi zimekua zikitumika bila usimamizi na kusababisha madhara makubwa kwa watumiaji.
kwa hapa tanzania tafiti zinaonyesha zaidi ya asilimia 70 ya wanawake hutumia dawa za kujichubua na huku asilimia mbili mpaka tano ya wanaume hutumia pia.
kuna aina tatu ya madawa hayo, dawa za kumeza, dawa za kupaka, dawaza kuchoma sindano na njia ya upasuaji lakini kwa hapa kwetu wengi hutumia za kupaka na wachache za kunywa.
watu wengi wamekua wakiiga wasanii wa nje kama marekani huku wakishindwa kujua kwamba wale pale wanafanya vile kwa usimamizi wa madaktari bingwa wa ngozi na kwa  dozi maalumu ili wasipate madhara yeyote.
serikali imekua ikijitahidi kuyapiga marufuku madawa hayo bila mafanikio kwani watu wengi huyapitisha na kuyatumia kwa magendo wakidhani wanaikomoa serikali bila kujua wanajiua wenyewe.
yafuatayo ni madhara yatokanayo na kujichubua ngozi..
kansa ya ngozi;dawa za kujichubua zina kemikali kuu mbili yaani hydroquinone na mercury, lakini dawa nyingi zinazopatikana mtaani zina mchanganyiko wa steroids, tretinion, na hydroquinone. kemikali hizi ni moja ya vyanzo vikuu vya kansa ya ngozi na kuharibu maini.


Kuongezeka kwa weusi wa ngozi;matumizi ya kemikali kama hydroquinone 2% kwa muda wa miezi mitatu mfululizo huweza kusababisha ngozi kua nyeusi zaidi na kukataa matibabu yeyote ya kuirudisha kwenye hali yake ya kawaida. lakini pia matumizi makubwa ya vipodozi hivi husababisha sehemu kama za vidole, miguu na masikio kua nyeusi zaidi kuliko sehemu zingine.
                                                      


Ngozi kua nyembamba sana; hii husababishwa na kemikali ambazo hupunguza sana unene wa ngozi, ngozi hii honyesha mishipa ya ndani ya damu na ni rahisi sana kuumia na kuvuja damu kirahisi.                                 
Vidonda visivyopona; kawaida ngozi ya mtu wa kawaida huweza kupona yenyewe ikiumia bila kutumia dawa yeyote lakini matumizi ya kemikali za kujichubua husababisha ngozi kupoteza uwezo wake wa kupona wenyewe.

Kuungua na mapele ya ngozi;kemikali hizi huweza kuunguza ngozi na kufanya iwe na mabaka baka, chunusi, harara na ngozi isiyokua na afya. kemikali ya hydroquinone hufanya kazi ya kuzuia ngozi kutengeneza kitu kinachoitwa melanin ambacho ni muhimu kwa ajili ya kuleta rangi ya ngozi.
                                          
Magonjwa ya ngozi; tafiti nyingi zilizofanywa na madaktari wa ngozi zimegundua kwamba watu wengi wanaosumbuliwa na magonjwa mbalimbali ya ngozi kama upele, miwasho, fangasi na aleji ni watu wanaotumia kemikali hizi hatari za kujichubua.
                                         

Huingiza sumu za ndani ya mwili; moja ya madhara makubwa ya kutumia kemikali za kuchubua rangi ya ngozi ni kuingiza sumu mwilini. sumu hizi huingia ndani ya mwili kupitia ndani ya ngozi, kwa vidonge vya kujichubua au sindano zinazotumika kwa kazi hii. madhara yake ni kuharibika kwa figo, kuharibika kwa ngozi, kinga ya mwili kushuka, kupata ngazi sehemu mbalimbali za mwili.
                                                      

Kubadilika kwa ngozi ya uso; hali hii hutokea pale ngozi ya uso inakua nyembamba sana kuliko sehemu zingine za mwili na husababisha kubadilika kwa ngozi ya uso na kua na hali tofauti kabisa.
                                                    

Kuathirika kisaikolijia; watu wengi waliojichubua na kupata madhara wanakosa amani wakiwa mbele za watu kwa kuhisi kwamba wanasemwa sana kulingana na hali yao ya sasa ilivyo, hii huwanyima uhuru na kuwafanya wawe watu wa kukaa ndani tu au kuvaa nguo za kuficha sura zao muda mwingi.
                                            
Kuharibu watoto tumboni; kemikali za kujichubua zina uwezo wa kuingia mpaka kwenye kizazi cha mama mjamzito, hali hii huweza kusababisha kuzaliwa kwa mtoto mwenye upungufu wa viungo fulani vya mwili kama mkono mmoja au mguu mmoja.


Upofu; kemikali za kuchubua ngozi ambazo hupakwa usoni zina uwezo wa kuharibu macho na kumfanya mtu awe kipofu kabisa, mimi binafsi nimeshuhudia watu waliopata upofu sababu ya kujichubua ngozi.



michirizi ya ngozi; kwasasa kuna wanawake wengi sana wanasumbuliwa na tatizo la michirizi ya ngozi, japokua michirizi hii huletwa na unene auujauzito lakini kujichubua pia moja ya vyanzo vikuu vya hali hii.

mwisho; kama wewe ndio unaanza kujichubua basi ujue uko kwenye hatari kubwa, inawezekana kwa sasa mambo yako ni safi kwamba umeshakua mweupe na kila mtu anakusifia lakini naomba nikwambie mbio zako za sakafuni zina ukingo..... kama umeshaathirika tayari basi ni wakati wa kuacha na kuomba msaada wa matibabu ili urudi kwenye hali yako ya kawaida. sasa hivi kuna kampuni nyingi za nje zinauza dawa kwa ajili ya matibabu ya waathirika wa hali hii.pia unaweza ukawasilaina na sisi na ukapata matibabu popote ulipo.

Bonyeza HAPA Kudownload Applicationi Ya Mawingu Blog Kwenye Simu Yako Ili Kupata Habari Zetu Haraka

===

Tupe Maoni Yako Hapa Chini
 

Mawingu Blog | Home Of Newz Copyright © 2017