Like Us On Facebook
Follow Us on Twitter

Jibu La Harmorappa Kuhusu Jinsia Yake Laibua Mshangao Mitandaoni

Mwanamuziki ambaye amekuja kwa kasi kwenye tasnia ya, Harmorappa au muite Kiboko ya Mabishoo leo amewaacha midomo wazi watu wengi kufuatia jibu lake alilolitoa alipoulizwa kuwa yeye ni mwanaume wa aina gani.
Akiwa katika kipindi cha Kikaangoni kinachorushwa na EATV, Harmorappa aliulizwa swali lililotumwa na shabiki aliyekuwa akifuatilia kipindi hicho ambalo liliuliza, “Wewe ni mwanaume wa aina gani?” na akijibu swali hilo alisema, “Mimi ni strong woman.”
Jibu hilo limewashangaza wengi kwa sababu Harmorappa ni mwanaume na hivyo wengi wameshindwa kuelewa kama alielewa swali liliuliza nini au alijibu kama utani.
Alipoulizwa kama anafahamu lugha ya Kiingereza, Harmorappa alisema anaielewa vizuri lakini tatizo ni kwenye kuongea.
Aidha, amesema kuwa kwa sasa hana mpango wa kujiendeleza kimasomo hasa kwenda chuo labda ajifunze zaidi lugha ya Kiingereza. Kuhusu suala la kujiunga WCB, alisema, “Siwezi kujiunga WCB hata kwa shilingi ngapi, Sizuzuki na hela, maana kama ni hela hata mimi mwenyewe ninazo.”
Bonyeza HAPA Kudownload Applicationi Ya Mawingu Blog Kwenye Simu Yako Ili Kupata Habari Zetu Haraka

===

Tupe Maoni Yako Hapa Chini
 

Mawingu Blog | Home Of Newz Copyright © 2017