Like Us On Facebook
Follow Us on Twitter

Kauli ya Nape Nnauye kuhusu CCM kwenye Sherehe za maadhimsho ya Muungano

Ikiwa leo Tanzania inatimiza miaka 53 toka Tanganyika na Zanzibar zilipoungana mwaka 1964 na kuunda nchi ya Tanzania Mbunge wa jimbo la Mtama, Mh Nape Nnauye amefunguka na kusema CCM ndiyo waasisi wa Muungano huo.

Mhe Nape Nnauye anakiri kuwa licha ya mapungufu ya hapa na pale katika chama chake hicho lakini bado kinabakia kuwa chama bora cha mfano barani Afrika, Nape Nnauye amesema hayo kupitia ukurasa wake wa Twitter

"CCM bado ni Chama bora cha mfano kwa Afrika! Ni imara na kina historia ndefu, nzuri iliyotukuka sana! Ndio waasisi wa Muungano Wetu, tuudumishe" alisisitiza Nape Nnauye




Bonyeza HAPA Kudownload Applicationi Ya Mawingu Blog Kwenye Simu Yako Ili Kupata Habari Zetu Haraka

===

Tupe Maoni Yako Hapa Chini
 

Mawingu Blog | Home Of Newz Copyright © 2017