Like Us On Facebook
Follow Us on Twitter

Msemaji wa Simba Aibeza Yanga Kwa Maneno Haya Baada ya Simba Kutoka Droo na Toto


Pamoja na Simba kupata sare ya bila kufungana dhidi ya Toto Africans, Msemaji wa Simba anaamini bado Simba ina nafasi ya kubeba ubingwa kwa kuwa iko kileleni kwa tofauti ya pointi sita.

Simba imefikisha pointi 62 na Yanga inafuatia ikiwa na pointi 56, hata hivyo Simba imecheza mechi 27 na Yanga ina pungufu miwili kwa kucheza 25.

Manara amesema: “Aliyenacho mkononi ni tofauti na anayesubiri kupata. Tuko kileleni kwa tofauti ya pointi sita, tusubiri kinachokuja. Ila niwaambie, nguvu za ubingwa ziko palepale.”

Bonyeza HAPA Kudownload Applicationi Ya Mawingu Blog Kwenye Simu Yako Ili Kupata Habari Zetu Haraka

===

Tupe Maoni Yako Hapa Chini
 

Mawingu Blog | Home Of Newz Copyright © 2017