Rapa huyo amedai huyo ni msanii wake wa kwanza wa kurap kwani siku chache zijazo atamtambulisha msanii wake wa kuimba.
“Leo label yangu ya ‘Free Nation 966’ imemtambulisha kijana wake wa kwanza ‘B Gway’,” alisema Nay. “Ni msanii mkali sana, sikutaka kumchukua msanii ambaye anatanisumbua, tena wimbo wake wa kwanza ‘Sijachukua’ amenishirikisha,”
Aliongeza, “Kwahiyo ningependa kuwaambia mashabiki wasubirie mambo mazuri kutoka ‘Free Nation 966’. Pia siku chache zijazo tutamtangaza msanii mwingine wa kuimba,”
Wimbo wa msanii huyo kuachiwa Jumatano hii kupitia redio na runinga pamoja na mitandaoni.
Bonyeza HAPA Kudownload Applicationi Ya Mawingu Blog Kwenye Simu Yako Ili Kupata Habari Zetu Haraka
===
Tupe Maoni Yako Hapa Chini