Like Us On Facebook
Follow Us on Twitter

Watoto 20 Wafariki Katika Ajali Afrika Kusini

Takriban watoto 20 wamefariki katika ajali ya barabarani katika mkoa wa Mpumulunga nchini Afrika Kusini kaskazini mwa mji mkuu wa Pretoria.

Kulingana na chombo cha habari cha Reuters, basi dogo walilokuwa wakisafiria liligonga lori na kulipuka.

Russel Meiring ,ambaye ni msemaji wa shirika la matibabu ya dharura ER24 ameambia Reuters kwamba watoto 20 walikuwa ndani ya basi hilo wakati lilipogongana na lori hilo la kubeba mizigo.
''Idadi hiyo sasa inadaiwa kufika 20'', alisema.

Chapisho la awali ambalo lilithibitisha watoto 13 kufariki ilionyesha eneo la ajli hilo.

Bonyeza HAPA Kudownload Applicationi Ya Mawingu Blog Kwenye Simu Yako Ili Kupata Habari Zetu Haraka

===

Tupe Maoni Yako Hapa Chini
 

Mawingu Blog | Home Of Newz Copyright © 2017