Askofu wa Kanisa la Ufufuo na Uzima, Josephat Gwajima amewaonya baadhi ya watu wanaoiongelea vibaya nchi akiwataka waache mara moja kwa kuwa wanachochea uvunjifu wa amani.
Askofu Gwajima amesema kinachotakiwa watu waizungumzie nchi vizuri kwa kuwa amani itakuwepo na uchumi wa nchi utaendelea kukua.
"Namkemea yule mtu ambaye anaiongelea vibaya nchi yetu huwezi ukawa unatoa kinywa kinachoashiria uvunjifu wa amani,"
"Huwezi kila siku unalaani kwa kuiongelea vibaya nchi yetu lazima nikemee ili nchi yetu iweze kuendelea kuwa na amani,"amesema Gwajima katika mahibiri kanisani kwake leo.
Bonyeza HAPA Kudownload Applicationi Ya Mawingu Blog Kwenye Simu Yako Ili Kupata Habari Zetu Haraka
===
Tupe Maoni Yako Hapa Chini


