Like Us On Facebook
Follow Us on Twitter

Video: Maalim Seif Afunguka Mambo Mazito Kuhusu Mgogoro Wa Cuf

Maalim seif
Katibu Mkuu wa Chama cha Wananchi (CUF), Maalim Seif Sharif Hamad amesema kuwa Msajili wa Vyama vya Siasa Nchini ndiye anayejaribu kupandikiza mgogoro ndani ya chama hicho kwa maslahi yake binafsi.

Ameyasema hayo mapema hii leo alipokuwa akizungumza katika kipindi cha 360 kinachorushwa na CloudsTv. kilichopo Jijini Dar es salaam.

Amesema kuwa hakuna haja ya wanachama kuwa na hofu kuwa chama hicho kinaweza kusambaratika hivyo amewataka kuimarisha mshikamano uliopo ndani ya chama hicho.

“Nachojua mimi hakuna mgogoro ndani ya CUF kama inavyoelezwa na baadhi ya watu, isipokuwa Msajili wa Vyama vya Siasa Nchini anajaribu kupandikiza mgogoro huo kwa maslahi yake binafsi,”amesema Seif.

Aidha, ameongeza kuwa kuna baadhi ya watu ambao wanatumiwa kutaka kukivuruga chama hicho, hivyo amesema kamwe hawatafanikiwa.

Hata hivyo, amesema yeye kama kiongozi ataendelea kufanya shughuli zake za chama na kuwataka walio chini yake wasivunjike moyo.
Tazama video hapa chini



Bonyeza HAPA Kudownload Applicationi Ya Mawingu Blog Kwenye Simu Yako Ili Kupata Habari Zetu Haraka

===

Tupe Maoni Yako Hapa Chini
 

Mawingu Blog | Home Of Newz Copyright © 2017