Baada ya msanii wa muziki wa asili nchini Mrisho Mpoto kumtaka rapa Afande Sele kuacha kumtaja marehemu Steven Kanumba kwa mambo mabaya, rapa huyo mwenye makazi yake mkoani Morogoro amemtaka Mrisho Mpoto kuacha mambo ya kizamani.
Wawili hao wamefikia hatua hiyo baada ya jana rapa Afande Sele kuandika ujumbe wa kusikitika baada ya kusikia Elizabeth Michael ‘Lulu’ kahukumiwa miaka miwili jela kwa kosa la kumuua aliyekuwa mpenzi wake, Steven Kanumba bila kukusudia.
Katika ujumbe wa Afande alidai yeye hakuhudhuria mazishi ya staa huyo wa filamu kwa madai alimsababishia Lulu matitizo kauli ambayo ilipingwa na Mrisho Mpoto kwa kudai marehemu hasemwi kwa mabaya.
Baada ya kauli hiyo, Afande Sele amerudi upya na kumjibu Mrisho Mpoto.
Bonyeza HAPA Kudownload Applicationi Ya Mawingu Blog Kwenye Simu Yako Ili Kupata Habari Zetu Haraka
===
Tupe Maoni Yako Hapa Chini