Like Us On Facebook
Follow Us on Twitter

Tundu Lissu Awapa Ujumbe Mzito Watakaoichagua CCM Kwenye Uchaguzi Dogo Wa Madiwani


Mbunge Singida Mashariki Tundu Antiphas Lissu ametuma ujumbe kwa wapiga kura kwenye kata zenye uchaguzi ya kwamba kuwapatia kura za ushindi Chama Cha Mapinduzi ni kufurahia na kuruhusu mateso.

Ujumbe huo kutoka kwa Lissu kwenda kwa wapiga kura umefikishwa na Diwani wa Sombetini  Arusha, Ally Bananga ambaye amefika hospitali ya Nairobi nchini Kenya anakopatiwa matibabu mbunge huyo.


Usipitwe na Habari Muhimu, Install App  Yetu

Android ===>  Bofya hapa

Kupitia ukurasa wake wa Instagram Bananga ameandika, "Nendeni mkawaambie watu kwenye kata zenye uchaguzi kuipa kura ccm ni kufurahia na kuruhusu mateso yetu yaendelee!!...."  Ujumbe alioutoa Lissu kupitia diwani Bananga

Ameongeza kwamba 'Hawa watesi wetu wako katika hatua za mwisho, kama wanajiamini kwa nn wanawawekea mizengwe wagombea wetu ili wao wapite bila kupingwa"



Bonyeza HAPA Kudownload Applicationi Ya Mawingu Blog Kwenye Simu Yako Ili Kupata Habari Zetu Haraka

===

Tupe Maoni Yako Hapa Chini
 

Mawingu Blog | Home Of Newz Copyright © 2017