Like Us On Facebook
Follow Us on Twitter

Haji Manara ataja Kilichomchukiza wakati Yanga ikiwatoa Ihefu FA cup

Moja kati ya Maafisa habari ambao wamekuwa na Mbwembwe hasa wanapopata nafasi ya Kuandika au Kuongea kuhusu Mpira Haji Manara wa Simba amekuwa Kivutio sana hasa anapoongelea Utani kwa Yanga na Kuisifia Klabu yake ya Simba.
Baada ya Mchezo kati ya Ihefu na Yanga ulioisha kwa Yanga kupata Ushindi kwa Penati 4 kwa 3 dhidi ya Ihefu ya Mbarali mkoani Mbeya Haji Manara kupitia ukurasa wake wa Instagram alionekana kuchukizwa na Maamuzi ya Refa wa mchezo huo.
Hata Nyani hutamani pilau,mbeleko za baadhi ya maamuzi ni kichefuchefu..ndio maana baadhi ya team zikienda kwenye international competitions wanatutia aibu tu…Ndegelec!!
Refa huyo msomaji wa kwataunit alitoa tuta dakika za Mwisho kabisa mara baada ya Obrey Chirwa kuangushwa kwenye eneo hatari akielekea Kufunga, Penati ambayo iliwekwa kambani na Obrey Chirwa.

Bonyeza HAPA Kudownload Applicationi Ya Mawingu Blog Kwenye Simu Yako Ili Kupata Habari Zetu Haraka

===

Tupe Maoni Yako Hapa Chini
 

Mawingu Blog | Home Of Newz Copyright © 2017