Mbunge wa Kawe Halima Mdee leo April 25, 2017 alisimama mbele ya bunge na kuomba msamaha ikiwa ni siku kadhaa tangu atuhumiwe kwa kosa la kumtukana spika wa Bunge Job Ndugai wakati mkutano wa bunge ukiendelea.
Mdee amesema…>>>’Nakiri kosa la kumtukana spika, nasema nilitenda kosa na nakiri kwamba sitorudia tena. Naamini kuna wanachi wengi niliwakwaza wakiwemo wapiga kura wangu.
‘Naahidi kuanzia sasa nitakuwa nikitoa michango yangu kwa kutumia lugha za staha!‘ –Halima Mdee
Bonyeza HAPA Kudownload Applicationi Ya Mawingu Blog Kwenye Simu Yako Ili Kupata Habari Zetu Haraka
===
Tupe Maoni Yako Hapa Chini