Manuwari hizo mpya zitakazojuulikana kama ‘Project 23E000E’ zitagharimu kiasi cha dola za kimarekani bilioni 17.5 kila moja na zinatarajiwa kukamilika mwaka 2030. Ripoti ya ‘state media’ ilieleza.
Manuwari hizo zinatarajiwa kutumia nguvu za nyuklia kujiendesha na zitakuwa na uwezo wa kubeba ndege za kivita 90 kwa wakati mmoja ikiwamo ndege mpya aina ya T-50. Ilieleza ripoti hiyo.
Professor Vadim Kozyulin ambaye ni mtaalamu wa masuala hayo, alikubali kuwa manuwari hizo zitajengwa kwa kuzingatia muundo wa zile za marekani za ‘USS Gerald R Ford’.
“Kitakuwa ni kiwanja cha ndege kinachoelea huku kikisindikizwa na meli nyingine za kivita” alisema Mr Kozyulin.
Manuwari hiyo mpya itakuwa na ukubwa sawa na viwanja vitatu vya mpira wa miguu.
Ndege zitakazobebwa na manuwari hiyo ni pamoja na MiG-29K jets, aina mpya ya ndege za Sukhoi PAK FA, pamoja na zile za T-50.
Bonyeza HAPA Kudownload Applicationi Ya Mawingu Blog Kwenye Simu Yako Ili Kupata Habari Zetu Haraka
===
Tupe Maoni Yako Hapa Chini