Kweli utawala wa awamu ya tano kiboko! Tofauti na miaka iliyopita ambapo mastaa mbalimbali hufanya kufuru katika kusherehekea kumbukumbu ya siku zao za kuzaliwa, Jumapili iliyopita, ambayo ilikuwa ni bethidei ya staa wa filamu, Elizabeth Michael ‘Lulu’, lakini haikufanyika.
Chanzo makini kilipolidokeza juu ya kutofanyika kwa shughuli hiyo, Tuliwasiliana na muigizaji huyo, lakini katika hali ya kushangaza, alitoa povu (kufoka) mno, akitaka watu kuachana na habari zake, kwa vile haziwahusu. Kwa miaka kadhaa iliyopita, Lulu aliadhimisha bethidei yake katika hoteli kubwa au kumbi zenye ‘akili’ zikiambatana na mbwembwe nyingi za ulaji na manywaji, lakini mwaka huu imekuwa kimya.
Ili kuujua ukweli, Tulimtafuta kwa njia ya simu Lulu ili kumsikia anazungumziaje kuhusu siku yake hiyo kubwa maishani mwake.
Haloo Lulu, hongera kwa kuongeza mwaka mwingine kwenye maisha yako.
Lulu: Asante sana.
Je, bethidei yako ulifanyia wapi maana mashabiki wako wanapenda kujua ilikuwaje?
Lulu: Hilo haliwahusu.
Kuna habari kwamba mwaka huu hujafanya sherehe kwa sababu ya ukata, hili likoje?
Lulu: Kama nimefanya au sijafanya linawahusu nini, kwanza kuanzia leo msinipigie simu tena, yaani sitaki kabisa simu zenu.
Sisi tulitaka tu kuujua ukweli kuhusu suala la kwamba ukata ndiyo umesababisha sherehe isifanyike.
Lulu akakata simu.
Hata hivyo, wakati Lulu akishindwa kufanya sherehe hizo Jumapili, jana yake, msanii wa Muziki wa Kizazi Kipya, Isabela Mpanda, alifanya bethidei yake katika Ukumbi wa Belinda uliopo Mbezi Beach.
Bonyeza HAPA Kudownload Applicationi Ya Mawingu Blog Kwenye Simu Yako Ili Kupata Habari Zetu Haraka
===
Tupe Maoni Yako Hapa Chini