Like Us On Facebook
Follow Us on Twitter

Mwakyembe Awashauri Wasanii Waache Kuimba Nyimbo za Siasa.......Asema Anayetaka Siasa Aache Mziki Akagombee Udiwani

Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dkt Mwakyembe amewasihi watanzania kuacha kutumiwa na viongozi mbalimbali kwa kuimba nyimbo za masuala ya kisiasa na badala yake wafanye kazi ambazo zitawasaidia kupata mafanikio.

Waziri Mwakyembe aliyasema hayo bungeni wakati akijibu hoja mbalimbali zilizotolewa na wabunge wakati wa kujadili hotuba ya bajeti ya wizara yake.

"Tembea dunia kote huko, nimekwenda Nigeria na kuona wasanii wakubwa kama Tiwa Savage, Don Jazz, Akon, P Square wale hawaimbi kuhusu viongozi wao wa kisiasa.


"Hivyo niwasihi wasanii wangu, muache kuimba kuhusu siasa sababu hii ni ‘entertainment industry’ (sekta ya burudani) na sio ya masuala ya kisiasa, "alisema Waziri Mwakyembe.

Aidha, waziri alisema kama kuna msanii yeyote anayetaka kuwa mwanasiasa aache muziki akagombee udiwani kwani wasanii waliotaka kuchanganya siasa na muziki walipotea kabisa.

Msikilize hapo chini  

Bonyeza HAPA Kudownload Applicationi Ya Mawingu Blog Kwenye Simu Yako Ili Kupata Habari Zetu Haraka

===

Tupe Maoni Yako Hapa Chini
 

Mawingu Blog | Home Of Newz Copyright © 2017