Like Us On Facebook
Follow Us on Twitter

Waziri Simbachawene Amuunga Mkono Rais Magufuli Kuhusu Kauli Ya Kuifuta Halmashauri Kama Madiwani Watalazimisha Kumfukuza Mkurugenzi


Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Mh. George Simbachawene amefunguka na kutetea kauli ya Rais magufuli aliyoitoa mkoani Kilimanjaro kuwa atafuta halmashauri hiyo kama madiwani watadiliki kutaka kumtoa Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo ambaye yeye amemteua.


Akitoa ufafanuzi bungeni Simbachawene amesema kuwa Rais Magufuli alitoa kauli hiyo kwa nia njema kwa kuwa wapo baadhi ya madiwani huwa wanataka kuwaondoa watendaji hao kwa maslahi yao binafsi na kusisitiza kuwa ikitokea hivyo hata kabla ya Rais hajachukua hatua ya kuvunja hiyo Halmashauri yeye ataanza kuivunja.

"Si kweli kwamba kauli ya Rais Magufuli imeleta mkanganyiko, ile kauli Rais amemaanisha pale unapokuwepo mkakati wa Madiwani kutaka kumuondoa Mkurugenzi wa halimashauri kwa maslahi yao binafsi, haya yote huwa yanatokea .

"Rais Magufuli hakusema kauli hiyo kuwalinda wabadhirifu bali pale unapokuwepo mpango mkakati wa madiwani kwa wakurugenzi kwa chuki, ikitokea hivi mimi mwenyewe nitaivunja hiyo halmshauri kabla hata Rais hajafanya maamuzi hayo" alisema Simbachawene

Bonyeza HAPA Kudownload Applicationi Ya Mawingu Blog Kwenye Simu Yako Ili Kupata Habari Zetu Haraka

===

Tupe Maoni Yako Hapa Chini
 

Mawingu Blog | Home Of Newz Copyright © 2017