Like Us On Facebook
Follow Us on Twitter

Baby Madaha Atoboa Siri Ya Namba 666 Kwenye Jina Lake

Mwanamuziki na muigizaji kutoka Bongo, Baby Madaha.
MWANAMUZIKI ambaye pia ni muigizaji kutoka Bongo, Baby Madaha ametoboa juu ya namba 666 ambayo anaitumia kwa sasa ikiwemo kwenye mitandao ya kijamii.

Akichonga na Star Mix, Baby Madaha alisema kuweka namba hiyo mbele ya jina lake inamaanisha haki, uwazi na usawa na si alama ya kishetani kama wengi wanavyofikiria.
“Watu wengi wanaamini namba 666 inamaanisha mambo ya kishetani, lakini ninaamini namba hii inamaanisha haki, usawa na uwazi, basi,” alisema Baby Madaha.

Alipobanwa juu ya vitabu vya Mungu kuizungumzia namba hiyo kuhusika na masuala ya kishetani alisema kuwa hana la kuongeza kwani anachoelewa ndicho anachomaanisha anapoitumia namba hiyo

Bonyeza HAPA Kudownload Applicationi Ya Mawingu Blog Kwenye Simu Yako Ili Kupata Habari Zetu Haraka

===

Tupe Maoni Yako Hapa Chini
 

Mawingu Blog | Home Of Newz Copyright © 2017