Like Us On Facebook
Follow Us on Twitter

Odinga Awatagazia Wafuasi Wake Kususia Bidhaa Za Kampuni Tatu Kenya

Kiongozi wa Muungano wa upinzani nchini Kenya National Super Alliance (Nasa), Raila Odinga.
Muungano wa upinzani nchini Kenya National Super Alliance (Nasa) umetoa wito kwa wafuasi wake kususia bidhaa na huduma kutoka kwa kampuni tatu ambazo unadai zimekuwa zikimpendelea Rais Uhuru Kenyatta.
Bw Kenyatta alitangazwa Jumatatu kuwa mshindi wa uchaguzi wa marudio uliofanyika 26 Oktoba, ambao kiongozi wa Nasa Raila Odinga alisusia akisema haungekuwa huru na wa haki.
Bw Odinga alitangaza kabla ya uchaguzi huo kwamba muungano huo utabadilika na kuwa Kundi la Pingamizi dhidi ya Serikali na baadhi ya hatua ambazo ulisema utachukua ni kususia bidhaa na huduma kutoka kwa kampuni ambazo alidai zinamfaa Bw Kenyatta.
Kampuni ambazo Nasa wamesema wafuasi wao wanafaa kususia ni:
•Kampuni ya mawasiliano ya Safaricom, ambayo ndiyo tajiri zaidi miongoni mwa kampuni za Kenya
Usipitwe na Habari Muhimu, Install App  Yetu


Android ===>  Bofya hapa
•Kampuni ya maziwa ya Brookside, inayomilikiwa na familia ya Kenyatta
•Kampuni ya kutengeneza mafuta ya kupikia na sabuni ya Bidco
Safaricom leo ilitangaza Safaricom kukua kwa faida yake baada ya kutozwa ushuru kwa kipindi cha nusu mwaka kilichomalizika tarehe 30 Septemba kwa asilimia 9.5 hadi Sh26.2 bilioni.
Kampuni hizo kufikia sasa hazijazungumzia hatua hiyo ya upinzani ya kuwataka Wakenya kususia bidhaa na huduma zao.
Bw Odinga alisusia kushiriki uchaguzi huo wa mwezi uliopita akishinikiza mageuzi yafanywe kwanza katika Tume ya Taifa ya Uchaguzi.
Uchaguzi huo ulitokana na hatua ya Mahakama ya Juu kufuta matokeo ya uchaguzi wa tarehe 8 Agosti ikisema ulikuwa na kasoro nyingi.
Mahakama hiyo ilikuwa inatoa uamuzi katika kesi iliyokuwa imewasilishwa na Bw Odinga kupinga matokeo hayo.
Bw Kenyatta alishinda uchaguzi huo wa marudio kwa kura 7.5 milioni ambazo ni sawa na asilimia 98 ya kura zilizopigwa.
Idadi ya waliojitokeza ilikuwa ni asilimia 38.84 ya waliokuwa wamejiandikisha kushiriki uchaguzi huo.
CREDIT: BBC SWAHILI
Matokeo kamili ya wagombea wote kama yalivyotangazwa na IEBC
MgombeaChamaKuraAsilimia
Uhuru KenyattaJubilee7,483,89598.28
Raila Odinga (Alisusia)ODM73,2280.96
Mohamed Abduba DidaARK14,1070.19
Japheth Kavinga KaluyuMgombea wa kujitegemea8,2610.11
Michael Wainaina MwauraMgombea wa kujitegemea6,0070.08
Joseph Nthiga NyagahMgombea wa kujitegemea5,5540.07
John Ekuru AukotThirdway Alliance21,3330.28
Cyrus JirongoUDP3,8320.05

Bonyeza HAPA Kudownload Applicationi Ya Mawingu Blog Kwenye Simu Yako Ili Kupata Habari Zetu Haraka

===

Tupe Maoni Yako Hapa Chini
 

Mawingu Blog | Home Of Newz Copyright © 2017