Like Us On Facebook
Follow Us on Twitter

Bunge Kufutilia Mbali Huduma Ya Obamacare Marekani

Bunge la marekani
Bunge la wawakilishi Marekani limepanga kura leo kufutilia mbali sheria ya huduma ya afya ya nafuu unaojulikana kama Obamacare.
Wanachama wa Republican wana imani kwamba sasa wana kura za kutosha.
Kevin McCarthy, kiongozi wa wengi bungeni amesema kwamba hatua muhimu imepigwa kuelekea kuidhinishwa mojawapo ya ahadi alizotoa rais Donald Trump wakati wa kampeni.
Kipengee kilichokarabatiwa kinachoahidi dola bilioni 8 kusaidia watu walio na magonjwa ya kitambo, kinaonekana kuwaridhisha waliokuwa na shaka.
Jitihada ya awali kufutilia mbali sheria hiyo mnamo Machi haikufaulu na ilikuwa mojawapo ya wakati mgumu wa siku mia moja za kwanza za rais Trump katika utawala.

Bonyeza HAPA Kudownload Applicationi Ya Mawingu Blog Kwenye Simu Yako Ili Kupata Habari Zetu Haraka

===

Tupe Maoni Yako Hapa Chini
 

Mawingu Blog | Home Of Newz Copyright © 2017