Like Us On Facebook
Follow Us on Twitter

Huu Ndo Ukweli Kuhusu Unywaji Wa Supu Ya Pweza Kuongeza Nguvu Za Kiume

HAMU ya tendo la ndoa kwa mwanadamu au mwanamke ni moja ya hisia za msingi kwa mtu wa kawaida kama ilivyo njaa au usingizi.
Kwa ajili ya matatizo mbalimbali yaliyo katika jumuiya, pamoja na kwamba tendo la ndoa ni jambo la msingi kwa wale waliooana, kuna wanaume aidha hawana uwezo wa kulifanya tendo hili au wana hisia ndogo na nguvu kidogo za kutekeleza tendo hili.
Panapokuwa na changamoto Fulani, wajasiriamali huiona changamoto hiyo kama fursa, na fursa hiyo imeonekana kuwanufaisha vijana wanaokaanga samaki aina ya pweza katika soko la samaki la kimataifa la magogoni baada ya supu ya samaki huyo aina ya pweza kuonekana kupendelewa sana na wanaume wa rika zote nchini.

Lakini siku za hivi karibuni hiki kitumbua kimonekana kuingia mchanga, yaani biashara kuharibika baada ya uvumi kwenye mitandao ya kijamii kudai kwamba wakaanga samaki wanaweka dawa za kuongeza nguvu za kiume aina ya viangra ili kuisisimua miili ya wateja wao, mwandishi wetu Austin Beyadi amezungumza na baadhi ya wakaanga pweza katika soko la samaki ili kupata ukweli kuhusu tuhuma hizo.
Mwenyekiti wa ukanda wa wakaanga samaki …………..amesema hakuna ukweli wowote wa wakaanga samaki kuweka madawa ya kuongeza nguvu bali vinaweka viungo vya kawaida kama anavyofafanua.
Ni imani ya wanaume wengi wa pwani na hata kutoka bara ambao huishi ukanda wa pwani siku hizi hupenda supu ya pweza kutokana na wingi wake wa virutubisho ambavyo huamini kuwa vinaongeza nguvu za kiume kwa waliopungukiwa.

Baadhi ya vijana waliozungumza na Clouds Tv wamedai kwamba mara nyingi wanatumia supu ya pweza ili kusisimua mwili huku wengine wakidai wanatumia kama kiburudishotu sio kama dawa ya kuongeza nguvu.
ULAJI wa supu ya pweza, kwa dai kwamba vinaongeza urijali kwa wanaume kumeelezwa kuwa ni dhana potofu inayostahili kupigwa vita kwa kuwa haina uhusiano kati ya urijali wa mwanaume na virutubisho vinavyotolewa na chakula hicho.
Kwa siku za hivi karibuni vijana wengi wameonekana kuchangamkia matumizi ya dawa za kuongeza nguvu za kiume bila kushauriwa na daktari, ANNA …… ni mfanyabiashara wa duka la dawa na hapa anaeleza wateja wake ni akina nani.


Bonyeza HAPA Kudownload Applicationi Ya Mawingu Blog Kwenye Simu Yako Ili Kupata Habari Zetu Haraka

===

Tupe Maoni Yako Hapa Chini
 

Mawingu Blog | Home Of Newz Copyright © 2017