Like Us On Facebook
Follow Us on Twitter

Wastara Amfungukia Mange Kimambi na Wanaomtuhumu Kuwa Tapeli


Msanii wa filamu wa bongo Wastara Juma ambaye hivi karibuni amepewa mchango wa milioni 15 na familia ya Rais Magufuli, amewajibu watu wanaomtuhumu kuwa tapeli kwani hana ugonjwa unaomsumbua.

Akizungumza na mwandishi wa www.eatv.tv Wastara amesema kabla ya kuomba michango alijitahidi sana kujitafutia mwenyewe hiyo pesa kwani hakutaka pesa ya mtu mwengine ije imsaidie, kwani alijiona anakuwa mzigo kwa jamii.

Kufuatia kauli hiyo Wastara amesema alishajaribu kujiingiza kwenye biashara ambazo amedai hazina faida, mpaka kufikia hatua ya kuanza kuuza vitu vya ndani, jambo ambalo msanii mwenzake Steve Nyerere alimkataza, na kumshauri aweke wazi matatizo yake iili watu wamsaidie.

Akiendelea kulalamikia kitendo cha watu kumdhihaki, amesema asilimia kubwa ya watu wanaomtuhumu hawajahi hata kwenda kumuona wakiwemo wasanii wenzake, ambao waliamua kumtenga baada ya yeye kuolewa na aliyekuwa Mbunge wa CCM Sadifa.

Baadhi ya wasanii wamesikika wakiongea chini chini kuwa Wastara anajidai kuumwa ili apate hela , pia Mwanadada Mange Kimambi amemlipua Wastara kupitia ukurasa wake wa Instagram 

Bonyeza HAPA Kudownload Applicationi Ya Mawingu Blog Kwenye Simu Yako Ili Kupata Habari Zetu Haraka

===

Tupe Maoni Yako Hapa Chini
 

Mawingu Blog | Home Of Newz Copyright © 2017