Like Us On Facebook
Follow Us on Twitter

Mavituz Ya Papy Tshishimbi Yazua Sekeseke Singida

Papy Tshishimbi.
WAKATI wapenzi na mashabiki wa soka mkoani Singida wakijiandaa kuiona kwa mara ya kwanza timu yao ya Singida United ikicheza kwenye uwanja wake wa nyumbani wa Namfua dhidi ya Yanga kesho Jumamosi, mashuti ya Papy Tshishimbi yamezua balaa ndani ya timu hiyo.

Jumamosi iliyopita, Tshishimbi alipiga mashuti mawili ya nguvu alipokuwa aki­itumikia Yanga dhidi ya Simba katika mch­ezo wa Ligi Kuu Bara uliofanyika kwenye Uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam. Hata hivyo mashuti hayo yalipanguliwa kwa ufanisi mkubwa na kipa wa Simba, Aishi Manula ambaye alifanya kazi kubwa katika mechi hiyo.

Kutokana na hali hiyo, viongozi wa Singi­da United wanaumiza vichwa vyao kila wa­napomfikiria kiungo huyo wa Yanga, am­baye hivi sasa ndiye gumzo kubwa hapa nchini kutokana na uwezo wake mkubwa alioonyesha dhidi ya Simba, Jumamosi iliyopita.Mkurugenzi wa Singida United, Festo San­ga, ameliambia Championi Ijumaa kuwa Tshishimbi ndiye mchezaji ambaye wan­amhofia zaidi katika mechi hiyo japokuwa wanaamini kuwa kocha wao mkuu raia wa Uholanzi, Hans van Der Pluijm atakuwa ameshamuandaa mtu maalumu wa kuka­biliana naye uwanjani.

“Sisi kama uongozi tumejipanga vizuri kwa ajili ya mechi hiyo lakini pia mambo yote ya kiufundi ndani ya uwanja, pia ko­cha wetu, Pluijm amejipanga vizuri.
“Hata hivyo, mchezaji ambaye tunam­hofia zaidi kwa upande wa Yanga ni Tsh­ishimbi kwani ni mchezaji mzuri tangu amejiunga na timu hiyo ndiye injini yao, tukifanikiwa kumdhibiti huyo basi kazi itakuwa nyepesi kwa upande wetu,” al­isema Sanga.

Hiyo itakuwa ni mara ya pili kwa timu hizo mbili kukutana mwaka huu, ambapo mara ya kwanza ilikuwa katika mchezo wa kirafiki kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam na Yanga iliibuka na ushindi wa mabao 3-2.

Wakati huohuo, Pluijm amezungumza na Championi Ijumaa juu ya mchezo huo am­bapo amesema: “Upande wetu sisi tuko vizuri kabisa na tupo tayari kwa ajili ya pambano hilo, na nina uhakika mkubwa kwamba tutaonyesha upinzani mkubwa kwa wapinzani wetu, kutokana na sisi kuwa nyumbani lakini tunawajua vyema wapinzani wetu.

“Tunaingia kwenye mechi hii tukiwa tuna­wajua vizuri wapinzani wetu kwa sababu wengi kabla ya kuja huku tulikuwa pale, kwa hiyo hapo kuna urahisi mkubwa wa sisi kupata matokeo mbele yao.”

Bonyeza HAPA Kudownload Applicationi Ya Mawingu Blog Kwenye Simu Yako Ili Kupata Habari Zetu Haraka

===

Tupe Maoni Yako Hapa Chini
 

Mawingu Blog | Home Of Newz Copyright © 2017