Moja ya story kubwa ambayo inaendelea kuwa gumzo na ku-make headlines kwa kuibua mijadala sehemu mbali ni kuhusu mavazi ya Jeans kwa waliookoka ambapo licha ya elimu kutolewa limeonekana kuwa gumu kwa baadhi ya watu.
Ayo TV imekutana na Mwimbaji staa wa Injili Tanzania, Christina Shusho ambaye anaeleza kama ni sahihi au sio sahihi kwa waliookoka kuvaa vazi la Jeans.
“Jeans si dhambi japo jamii yetu bado baadhi yao hawataki kukubali. Bado wameshikilia sheria ile kwamba ni dhambi na mimi naamini kuna baadhi ya Wachungaji, Watumishi wa Mungu ambao nimezungumza nao wanafahamu ukweli kwamba si dhambi lakini shida ni walishaaminisha Waumini kwamba suruali ni dhambi.” – Christina Shusho.
Bonyeza HAPA Kudownload Applicationi Ya Mawingu Blog Kwenye Simu Yako Ili Kupata Habari Zetu Haraka
===
Tupe Maoni Yako Hapa Chini

