Like Us On Facebook
Follow Us on Twitter

Aliyefanikisha Kukamatwa Malkia Wa Pembe Za Ndovu Kauawa Kwa Risasi Dar

Mpelelezi kinara aliyefanikisha kukamatwa kwa Yang Feng Glan maarufu kama ‘Malkia wa Meno ya Tembo’Wayne Lotter ameuawa kwa risasi na watu wasiojulikana.
Taarifa iliyochapishwa na mtandao wa The Guardian imesema kuwa Wayne Lotter, 51, alipigwa risasi Jumatano jioni katika maeneo ya Masaki, Dar es Salaam wakati akitokea Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere ambapo taxi alilopanda lilisimamishwa na gari lingine kabla ya watu wawili kutelemka na kumpiga risasi.
Lotter alikuwa Mkurugenzi na mwanzilishi-mwenza wa PAMS Foundation, Shirika lisilo la Kiserikali ambalo linajihusisha na masuala ya kupinga Ujangili ambalo lilianza shughuli zake Tanzania mwaka 2009 na mara kadhaa amekuwa akipokea vitisho vya kifo.

Bonyeza HAPA Kudownload Applicationi Ya Mawingu Blog Kwenye Simu Yako Ili Kupata Habari Zetu Haraka

===

Tupe Maoni Yako Hapa Chini
 

Mawingu Blog | Home Of Newz Copyright © 2017