Like Us On Facebook
Follow Us on Twitter

Chid Benz Amvuta Jay Z, Asema ile ya 2PAC Alikua Anatania, Ukweli ni huu

Baada ya sakata la kusema amefanya collabo na Tupac na kuleta mtafaruku mkubwa kwa mashabiki huku wakimtolea maneno makali wakisema amesha athirika kiakili kwa madawa ya kulevya kwa kuwa Tupac ni marehemu, sasa Chid Benz kuja na collabo na Jay Z.

Akifanya mahojiano kwenye kipindi cha Friday Night Live kinachorushwa na East Africa Television and Radio, Chid Benz amesema Collabo hiyo ameifanya na Jay Z huku 'chorus' yake ikifanywa na mke wa msanii hyo Beyonce, lakini anataka atoe 'chorus' hiyo na amuweke msanii wa Bongo Linah Sanga.

Chid Benz aliendelea kusema kuwa kauli hiyo anaitoa akiwa yuko sawa na sio mtu aliyelewa na madawa ya kulevya, na kwamba collabo hiyo imeshafanyika na cd yake ipo nyumbani kwa mama yake 'Mama Chid'.

 VIDEO: 

Bonyeza HAPA Kudownload Applicationi Ya Mawingu Blog Kwenye Simu Yako Ili Kupata Habari Zetu Haraka

===

Tupe Maoni Yako Hapa Chini
 

Mawingu Blog | Home Of Newz Copyright © 2017