Aliyewahi kuwa Mkuu wa Wilaya ya Handeni mkoani Tanga na mwandishi wa habari, Muhingo Rweyemamuamefariki dunia leo Jumamosi, Septemba 2.
Taarifa za kifo hicho zimethibitishwa na aliyekuwa Mwenyekiti Jukwaa la Wahahariri Tanzania, ambaye pia alikuwa rafiki wa karibu wa marehemu, Absalom Kibanda.
Katika utumishi wake, Muhingo Rweyemamu aliwahi pia kuwa mkuu wa wilaya za Morogoro, Makete na Mhariri Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya New Habari (2006) Limited.
Taarifa zaidi za msiba huo endelea kufuatilia habari kwenye mitandao yetu ya;
Bonyeza HAPA Kudownload Applicationi Ya Mawingu Blog Kwenye Simu Yako Ili Kupata Habari Zetu Haraka
===
Tupe Maoni Yako Hapa Chini