LWANDAMINA NDANI YA NYUMBA LEO
Klabu ya Yanga leo Jumatatu kwanza kabisa kocha wake mkuu George Lwandamina anatarajiwa kurejea nchini mara baada ya Kumaliza kuhani msiba kwao nchini Zambia tayari kwaajili ya Maandalizi ya mechi dhidi ya Mbeya City Jumapili ya wiki Hii.
Lwandamina ambaye aliondoka nchini mara baada ya mchezo kati ya Yanga na Singida United ambapo mchezo huo ulimalizika kwa sare ya bila kufungana, anarejea kwaajili ya michezo ya Ligi na kuanza kukamilisha masuala ya usajili wakati wa dirisha dogo.
MA- PRO NAO KUREJEA MAZOEZINI LEO
Wachezaji wa Kimatifa wa Yanga Obrey Chirwa na Tshishimbi wanatarajiwa kuanza mazoezi kufautia mara ya mwisho kutoonekana mazoezini kwasababu mbalimbali, Yanga leo watakuwa na mazoezi ya Gym kama ilivyoutaratibu wao wa kufanya mazoezi ya Gym kila Jumatatu na Kuendelea na mazoezi ya uwanjani siku za kawaida.
Ngoma naye msomaji wa kwataunit.com huenda Akarejea leo nchini kutoka kwao nchini Zimbabwe ambapo inadaiwa alikwenda kutibiwa ila akilaumiwa kwa kosa la kuondoka bila kuaga uongozi, japo kuna taarifa zinadai alimuaga kocha mkuu George Lwandamina.
Bonyeza HAPA Kudownload Applicationi Ya Mawingu Blog Kwenye Simu Yako Ili Kupata Habari Zetu Haraka
===
Tupe Maoni Yako Hapa Chini


