Like Us On Facebook
Follow Us on Twitter

Irene Huyo Na Dogo Janja Madee Atoa Kauli,Asema Hata Mwaka Hawatamaliza

Msanii Madee Seneda ambaye ni baba mlezi wa Dogo Janja, amewataka maharusi wake Irene Uwoya na Dogo Janja kutosikiliza watu kwani wakifanya hivyo hata mwaka hawatamaliza.
Madee ameyasema hayo alipokuwa akipiga stori na Queen Fifi na JR kwenye Planet Bongo ya East Africa Radio, na kusema kwamba amefurahi kuona Dogo Janja kaoa ingawa alishtushwa na taarifa hizo, lakini kikubwa ni kuwaombea ili wasisikilize maneno ya watu.

Madee ameendelea kusema kwamba wawili hawa wote ni watu maarufu hivyo kutakuwa na maneno mengi kutoka kwa watu, na iwapo wakisikiliza basi ndoa yao haitafika mbali.

Bonyeza HAPA Kudownload Applicationi Ya Mawingu Blog Kwenye Simu Yako Ili Kupata Habari Zetu Haraka

===

Tupe Maoni Yako Hapa Chini
 

Mawingu Blog | Home Of Newz Copyright © 2017